Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (MB) leo 19, Mei 2025 ameweka jiwe la Msingi kwenye jengo la Utawala la Halmashauri ya Buchosa ambalo liko katika hatua ya ukamilishaji,fedha shilingi Bilioni 4.3 zimepokelewa kwa awamu tofauti kakamilisha ujenzi wa jengo hilo.
Katika ziara hiyo Waziri Mkuu amekutana na kuongea na wananchi wa Kata Nyehunge na maeneo jirani ambapo amesema kwamba Serikali kazi yake ni kuwahudumia na kuwatumika wananchi katika kutekeleza shughuli mbalimbali miradi ya maendeleo.
“Leo nimeenda kuweka jiwe la msingi kwenye jengo letu ni jengo lililokamilika zaidi ya asilimia 80 bado maboresho madogo madogo kuwekwa vizuri ili lije kuzinduliwa rasmi” Mhe.Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa.
Katika hatua nyingine Mheshimiwa Majaliwa amewataka wazazi kupeleka Watoto wao vyuo vya Michezo. VETA, ili wapate ujuzi ambao utawasaidia kupata utaalamu mbalimbali ukiwemo utalaam wa michezo.
Amesema Serikali itaendelea kuleta fedha kujenga miundombinu ya madarasa ili kuondoa msongano kwenye shule zenye wanafunzi wengi, pamoja na kujenga mabweni na nyumba za Walimu.
Aidha ameeleza na kufafanua kwamba Serikali imeanza kutoa vibali vya ajira mbali mbali ikiwemo sekta ya Elimu na Afya lakini pia Serikali itaendelea kujenga Zahanati Pamoja na Vituo vya Afya maeneo yenye upungufu.
Buchosa District Council
Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA
Simu: 0759941297
Simu ya kiganjani: 0765029662
Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa