• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe |
Buchosa District Council
Buchosa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Misitu
    • Biashara
    • Ushirika
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Telesenta
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi idhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

KATIBU TAWALA SENGEREMA AHIMIZA WA SHERIA YA BIMA YA AFYA KWA WOTE BUCHOSA

Posted on: January 5th, 2026



Katibu Tawala Wilaya ya Sengerema, Bw. Cuthberth Midala, amehimiza umuhimu wa Bima ya Afya kwa Wote kwa lengo la kutoa elimu, kupokea maoni na kuimarisha uelewa wa jamii kuhusu manufaa ya bima ya afya katika Halmashauri ya Buchosa.


Akizungumza leo Januari 05, 2026 katika mkutano maalum na Watendaji wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Bw. Midala amesema utekelezaji wa sheria hiyo unalenga kuwawezesha wananchi kupata huduma bora za afya bila vikwazo, huku akisisitiza umuhimu wa jamii kujiunga na bima hiyo kwa maendeleo ya afya zao.

Katika mkutano huo, imeelezwa kuwa NHIF itaendelea kuwasajili wanachama waliokuwa wakitumia ICHF kupitia kifurushi cha huduma muhimu cha shilingi 150,000, ambapo watapatiwa namba za utambuzi za NHIF zitakazounganishwa na ICHF ili waendelee kupata huduma bila usumbufu.


Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Buchosa, Dkt. David Mndeba, amefafanua kuwa kuna vifurushi mbalimbali vya bima ya afya kwa mtu mmoja mmoja na kwa makundi maalum kama wachimbaji wa madini, bodaboda, wafanyabiashara na makundi mengine.


Ameeleza kuwa kaya inajumuisha watu sita baba, mama na watoto wanne na kifurushi cha jamii cha shilingi 150,000 kinahusisha huduma 372, bila kujali kaya ina mtu mmoja au sita.


Aidha, mkutano huo umejadili ulipaji wa madai kwa vituo vya kutolea huduma za afya na kusisitiza umuhimu wa kutoa huduma kwa usawa kwa wagonjwa wote bila ubaguzi kati ya wanaotumia bima na wanaolipa fedha taslimu.


Mkutano huo umehudhuriwa na makundi mbalimbali yakiwemo viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya ushirika, mama lishe, bodaboda pamoja na wenyeviti wa zahanati na vituo vya afya.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 27, 2025
  • TANGAZO NAFASI ZA AJIRA HALMASHAURI YA BUCHOSA November 25, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA MUDA YA UCHAGUZI November 20, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA October 13, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KATIBU TAWALA SENGEREMA AHIMIZA WA SHERIA YA BIMA YA AFYA KWA WOTE BUCHOSA

    January 05, 2026
  • MADIWANI BUCHOSA WAAPISHWA, RASMI KUANZA MAJUKUMU YA KUWATUMIKIA WANANCHI

    December 04, 2025
  • DED MIHAYO AWATAKA WATUMISHI KUFANYA KAZI KWA BIDII,KUDUMISHA AMANI

    November 28, 2025
  • WATUMISHI AJIRA MPYA WAPATIWA MAFUNZO BUCHOSA

    November 19, 2025
  • Angalia zote

Video

UTOAJI WA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUCHOSA
Video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Mpango Mkakati Wa Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Mkoa wa Mwanza
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA)
  • Wizara ya Kilimo

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Buchosa District Council

    Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA

    Simu: 0759941297

    Simu ya kiganjani: 0765029662

    Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa