• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe |
Buchosa District Council
Buchosa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Misitu
    • Biashara
    • Ushirika
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Telesenta
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi idhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MADIWANI BUCHOSA WAAPISHWA, RASMI KUANZA MAJUKUMU YA KUWATUMIKIA WANANCHI

Posted on: December 4th, 2025

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa latoa mikakati ya kuwatumikia wananchi ikiwa kipaumbele ni kuhakikisha ukusanyaji wa mapato unaongezeka.


Katika mkutano wa kwanza wa baraza hilo, Waheshimiwa Madiwani wamefanya uchaguzi wa viongozi katika kamati mbalimbali ambapo Mhe. Isaac Mashimba, Diwani wa Kata ya Kalebezo amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa naye Mhe. Samike Hezron, Diwani wa Kata ya Luharanyonga, amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti.

Mhe.Mashimba amewashukuru waheshimiwa madiwani mara baada ya kuchaguliwa kwa kura zote za ndiyo  kwa imani waliyoonyesha na kuahidi kuwa kiongozi atakayefika moja kwa moja kwa wananchi kusikiliza na kuwasilisha kero zao.Ameahidi Baraza hilo kwamba atahakikisha rasilimali zinasimamiwa vizuri na kwa usawa sambamba na hilo atahakikisha anasimamia maslahi ya wananchi na watumishi kwa ujumla.  

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mhe.Erick Shigongo amewashukuru Waheshimiwa Madiwani,Mkurugenzi Mtendaji na Watumishi kuwa wamoja kipindi cha uchaguzi hadi kufikia leo na kuahidi kutoa ushirikiano  kwa maslahi ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa ameeleza na kufafanua kwamba atashirikiana na waheshimiwa Madiwani katika kuhakikisha kuwa uchumi imara na endelevu  na jamii iliyoelimika yenye maisha bora na inayowajibika katika maendeleo.

“Sisi ni wanabuchosa tutaijenga wenyewe,nimekuja Buchosa kutoa huduma na si kutawala”Amesisitiza Bw.Mihayo.


Mkutano wa kwanza wa baraza la Madiwani umehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu Tawala Wilaya ya Sengerema Bw.Cuthbert Midala, viongozi wa vyama vya siasa, wakuu wa idara na Vitengo na wadau kama NMB na CRDB pamoja na wananchi.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 27, 2025
  • TANGAZO NAFASI ZA AJIRA HALMASHAURI YA BUCHOSA November 25, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA MUDA YA UCHAGUZI November 20, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA October 13, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MADIWANI BUCHOSA WAAPISHWA, RASMI KUANZA MAJUKUMU YA KUWATUMIKIA WANANCHI

    December 04, 2025
  • DED MIHAYO AWATAKA WATUMISHI KUFANYA KAZI KWA BIDII,KUDUMISHA AMANI

    November 28, 2025
  • WATUMISHI AJIRA MPYA WAPATIWA MAFUNZO BUCHOSA

    November 19, 2025
  • JITOKEZE KUPIGA KURA TAREHE 29 OKTOBA 2025

    October 05, 2025
  • Angalia zote

Video

UTOAJI WA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUCHOSA
Video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Mpango Mkakati Wa Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Mkoa wa Mwanza
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA)
  • Wizara ya Kilimo

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Buchosa District Council

    Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA

    Simu: 0759941297

    Simu ya kiganjani: 0765029662

    Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa