• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe |
Buchosa District Council
Buchosa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Misitu
    • Biashara
    • Ushirika
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Telesenta
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi idhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Vikundi 81 vya Wanawake,Vijana na Watu wenye ulemavu wapatiwa Mkopo wa asilimia 10 Buchosa

Posted on: March 12th, 2025


Vikundi vya Wanawake,Vijana na Watu wenye ulemavu wapatiwa mkopo wa thamani ya shilingi 460,000,000.00 katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa Mkoani Mwanza.

Hayo yamejiri leo tarehe 12, Machi,2025 wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya wawakilishi wa vikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu vilivyopatiwa mkopo wa asilimia 10 ambapo mgeni rasmi alikuwa Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mhe.Erick Shigongo.

Mhe.Erick Shigongo amewataka viongozi hao wa  vikundi kuzingatia nidhamu ya matumizi ya fedha,muda na kujituma kwa bidii ili kupata matokeo Chanya katika biashara zao na kuongeza kipato kwa familia.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo ameeleza na kufafanua kwamba kuna umuhimu wa wajasiriamali kuwa na kila sababu ya kuuchukia umaskini,kutafuta matatizo yaliyopo kwenye jamii na kuyatafutia ufumbuzi sambamba na kufanya kazi kwa juhudi ili waweze kufanikiwa katika shughuli  wanazifanya katika vikundi vyao.

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa ambaye pia ni Afisa Elimu Sekondari Bw.Simbanilo Changiki ametoa wito kwa wajasiriamali hao kusimamia malengo ambayo wamejiwekea ambapo wataweza kufikia mafanikio waliyoyakusudia, sambamba na kurejesha mikopo hiyo ambayo haina riba kwa wakati ili vikundi vingine  vyenye sifa viweze kukopa fedha hizo.

Katika vikundi 81 vya Wanawake,Vijana na Watu wenye ulemavu vimeweza kunufaika na mkopo wa asilimia 10 kwa mchanguo ufuatao ambapo vikundi 47 ni vikundi vya wanawake shilingi 208,500,000.00,vikundi 30 ni vijana shilingi 231,000,000.00 na vikundi 4 ni vya watu wenye ulemavu shilingi 20,500,000.000 na kufanya jumla shilingi 460,000,000.00 ambazo zimekopeshwa.

 Aidha lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wa kimkakati wa namna ya usimamizi na uendeshaji wa biashara wanazozifanya katika vikundi hivyo.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA UMMA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 26, 2024
  • MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KWA AJILI YA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA(BVR)-2024 August 02, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA July 17, 2024
  • TANGAZO LESENI ZA BIASHARA 2024 July 10, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Waziri Mkuu Apongeza Mradi wa jengo la Utawala,Aweka jiwe la msingi

    May 19, 2025
  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • DC Ngaga asisitiza Mahusiano mazuri kazini Buchosa

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

UTOAJI WA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUCHOSA
Video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Mpango Mkakati Wa Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Mkoa wa Mwanza
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA)
  • Wizara ya Kilimo

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Buchosa District Council

    Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA

    Simu: 0759941297

    Simu ya kiganjani: 0765029662

    Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa