• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe |
Buchosa District Council
Buchosa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Misitu
    • Biashara
    • Ushirika
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Telesenta
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi idhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

"Tupige vita Uvuvi haramu kwa Vitendo na si kwa maneno" Naibu Katibu Mkuu Dkt.Mhede

Posted on: December 21st, 2024

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi amewataka wananchi kuacha kutumia Uvuvi haramu wakati wa kuvua mazao ya Samaki katika Halmashauri ya Wilaya Buchosa Mkoani Mwanza.

Kauli hiyo imetolewa leo Jumamosi 21, Disemba,2024 na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt.Edwin Paul Mhede wakati wa ziara yake ya siku moja ya kutembelea na kukagua mradi wa Mwalo wa Samaki na dagaa Kanyala na Ujenzi wa soko la Samaki Nyakaliro ambapo ameridhishwa na hatua za ujenzi huo.

Dkt.Mhede amefafanua na kueleza kwamba kuna tabia ya baadhi ya wananchi ya kutumia njia ambazo hazikubaliki katika kuvua mazao ya samaki,waache kufanya hivyo na badala yake watumie njia ambazo zinakubalika ili kuondokana na uvuvi haramu.

“Hili jambo tushirikiane wote tusilipinge kwa kuongea peke yake,pia tulipinge kwa vitendo na inapotokea wachache miongoni mwetu ni vizuri wakaelimishwa kuwa jambo hili si zuri  na jambo hili linakemewa vikali na vyombo vyote” amesema Naibu Katibu Mkuu Dkt Mhede.

 Sambamba na hilo amesisitiza kwamba kwa mtu yeyote atakayebainika anajishughulisha na uvuvi haramu atachukuliwa hatua za kisheria ili kukomesha tabia hiyo ambayo haikubaliki hata kidogo.

Aidha Naibu Katibu Mkuu amesema kwamba Serikali inatoa mikopo ya asilimia 10 kupitia Halmashauri ambapo kupitia vikundi mbalimbali wanaweza kunufaika na mikopo hiyo isiyokuwa na riba na hasa kwa watu ambao wataamua kuwekeza kwenye ufugaji wa samaki kwa kutumia vizimba.

“Moja ya eneo ambalo ni uhakika ukiwekeza pesa inarudi na ninaiona ni ufugaji wa Samaki kwa kutumia njia ya vizimba”Amesisitiza Dkt.Mhede.

Hata hivyo,kupitia Mwalo wa Kanyala  Samaki aina ya sangara tani 217 na dagaa tani 774 huvuliwa kila mwaka, ambapo samaki na dagaa hutokea katika mialo ya Kanyala,Kasalazi,Gembale,Zilagula,Chembaya,Soswa na Yozu.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA UMMA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 26, 2024
  • MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KWA AJILI YA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA(BVR)-2024 August 02, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA July 17, 2024
  • TANGAZO LESENI ZA BIASHARA 2024 July 10, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • DC Ngaga asisitiza Mahusiano mazuri kazini Buchosa

    April 03, 2025
  • DED Benson Mihayo awataka watumishi kushirikana katika ukusanyaji Buchosa

    March 27, 2025
  • Angalia zote

Video

UTOAJI WA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUCHOSA
Video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Mpango Mkakati Wa Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Mkoa wa Mwanza
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA)
  • Wizara ya Kilimo

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Buchosa District Council

    Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA

    Simu: 0759941297

    Simu ya kiganjani: 0765029662

    Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa