• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe |
Buchosa District Council
Buchosa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Misitu
    • Biashara
    • Ushirika
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Telesenta
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi idhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Serikali yatenga eneo zaidi ya Hekta elfu mbili kwa Wananchi Kisiwa cha Maisome

Posted on: September 15th, 2024

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Dunstan Kitandula amewataka wananchi wa Kisiwa cha Maisome kifuata taratibu zilizowekawa na Serikali ili kulinda msitu wa asili wa  Maisome usitoweke na kuleta athari za amabadiliko ya tabia nchi.

Kauli hiyo imetolewa jana Jumamosi 14,Septemba,2024 na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Dunstan Kitandula alipofanya ziara ya siku moja  kwenye  Kisiwa cha Maisome alipokuwa akizungumuza na wananchi juu ya adhima ya Serikali  kuridhia ombi la wananchi wa kisiwa cha Maisome kupatiwa hekta 2,871.782 kwa ajili ya matumizi  ya shughuli mbalimbali za kijamii.

 "Msitu wa Maisome una hekata zaidi ya 12000 wananchi wamepewa hekta 2871 hivyo utabakiwa na Hekta 9319” amesema Naibu Waziri Kitandula.

Aidha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii amesema Serikali imeweka taratibu za wananchi kuokota kuni kwa ajili ya kupikia kwenye hifadhi ya msitu huo hivyo jamii inatakiwa kufuata taratibu zilizoweka za kuokata kuni mara tatu kwa wiki kwa angalizo la kutokukata miti ambayo ipo ndani ya hifadhi hiyo.

Kwa upande wake Mbunge wa Buchosa Eric Shigingo alieza na kufafanua kwamba kiu ya wanabuchosa wa Kata ya Maisome nikuona wanapiganiwa katika suala zima la maendeleo.

Shigongo amesema ilikuwa ni ajenda yake ambayo alitaka ifike mwisho ili kila wananchi wa Buchosa aweze kunufaika na rasimali za nchi huku akiwataka wananchi kuendelea kukiunga mkono chama cha Mapinduzi ambayo sera yake ni  kila mtanzania apate haki katika nchi hii.

"Nilisimamia ajenda hiyo Bungeni na Serikali imesikia kilio cha wananchi asante sana Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwaona wananchi wa Kata ya Maisome Buchosa” amesisitiza” Shigongo.

Naye Bakari Mohamed Meneja TFS Kanda ya Ziwa amefafanua kwamba wamepokea maelekezo ya Serikali hivyo wanachosubiria na mchakato wa kishireia ukamilike ili wananchi wakabidhiwe maeneo waliyopewa na Serikali.

Lukomwa Maendeka ni mkazi wa kisiwa cha Maisome amesema wamekuwa na changamoto ya kukosa maeneo ya malisho ya mifugo hali iliyopelekea mifungo yao kwenda hifadhini ambapo wamekuwa wakitozwa faini kubwa kati ya Shilingi 50,000 hadi Shilingi 100,000 pindi mifugo inapoingia hifadhini hapo na kupelekea baadhi ya wananchi kuuza mifugo yao.

Naibu Waziri wa Maliasli na Utalii Mhe.Dunstan Kitandula akiwasili katika Kisiwa cha Maisome na kupokelewa na mwenyeji wake Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mhe.Eric Shigongo mapema jana wakati wa ziara ya kutembelea hifadhi katika Kisiwa cha Maisome na kuongea wananchi.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA UMMA October 13, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA ASILIMIA 10 October 01, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MPIGA KURA 2025 September 17, 2025
  • TANGAZO LA KAZI YA MKATABA September 03, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • JITOKEZE KUPIGA KURA TAREHE 29 OKTOBA 2025

    October 05, 2025
  • WATHIBITI UBORA WA SHULE WAPATIWA MAFUNZO BUCHOSA

    September 30, 2025
  • DC NGANGA AWATAKA WATENDAJI WA KATA KUONGEZA JUHUDI UPATIKANAJI WA CHAKULA SHULENI

    September 17, 2025
  • BOTI TATU ZA THAMANI YA MILIONI 400 ZA POKELEWA BUCHOSA

    August 29, 2025
  • Angalia zote

Video

UTOAJI WA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUCHOSA
Video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Mpango Mkakati Wa Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Mkoa wa Mwanza
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA)
  • Wizara ya Kilimo

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Buchosa District Council

    Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA

    Simu: 0759941297

    Simu ya kiganjani: 0765029662

    Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa