• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe |
Buchosa District Council
Buchosa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Misitu
    • Biashara
    • Ushirika
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Telesenta
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi idhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

RAS Mwanza awataka wananchi Kuitunza na Kuilinda Miundombinu ya Ujenzi wa Miradi Wilayani Buchosa

Posted on: September 13th, 2024

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza awataka wananchi kutunza na kulinda miundombinu mbalimbali ambayo Serikali inatumia fedha nyingi katika kutekeleza miradi ya Maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa Mkoani Mwanza.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw.Elikana Bulandya ameyasema hayo tarehe 13, Septemba, 2024 wakati wa ziara yake ya kutembelea na kukagua miradi akiwa katika Kituo cha Afya Nyakasungwa ambapo ameeleza na kufafanua kwamba wananchi wanao wajibu wa kutunza miundombinu ya ujenzi wa miradi katika maeneo yao yanayowazunguka kwani Serikali inatoa fedha nyingi kujenga miradi hiyo ya maendeleo ili wananchi waweze kunufaika na kupata hudama bora na kwa wakati.

Aidha Bw.Bulandya ameeleza kufafanua kwamba mradi wa ujenzi wa Kituo  cha Afya cha Nyakasungwa ambacho kimejengwa kwa Mapato ya ndani ya Halmashauri kitakapokamilika kitaboresha huduma za afya kwa wananchi na kupunguza vifo vya watoto chini cha wa miaka 5,kupunguza vifo vya kinamama wajawazito na kitasaidia kupunguza umbali mrefu kwa wananchi kufuata huduma.

Katika hatua nyingine Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza ametembelea na kujionea hatua wa Ujenzi wa Vyumba viwili vya madarasa pamoja na matundu sita ya vyoo katika Shule ya Msingi Nyehunge iliyopo Kata ya Nyehunge, sambamba na miiradi mingine ambayo ni Ujenzi wa Mradi wa umwagiliaji Sukuma uliopo kijiji cha Sukuma Kata ya Bukokwa,Mradi wa Vijana (Toroka uje) uliopo Kata ya Nyakalilo na Mradi wa tenki la maji Nyakalilo.

Hata hivyo Katibu Tawala wa Mwanza ametoa maelekezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema kuwa Miradi yote ambayo itatembelewa na Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2024 kuwepo na nyaraka mbalimbali muhimu za miradi zikiwa zimepangwa vizuri sambamba na kukamilisha mapungufu ambayo yamejitokeza wakati wa ukaguzi wa miradi hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe.Senyi Ngaga ameeleza kwamba ameyapokea maelekezo hayo ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza na kuahidi kuyafanyia kazi ikiwa ni pamoja kuandaa nyaraka muhimu na kurekebisha kasoro ambazo zimejitokeza katika miradi hiyo.

 

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA UMMA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 26, 2024
  • MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KWA AJILI YA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA(BVR)-2024 August 02, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA July 17, 2024
  • TANGAZO LESENI ZA BIASHARA 2024 July 10, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MASHIRIKA YASIYO YA SERIKALI YAASWA KUENDELEA KUTOA MICHANGO KWA JAMII.

    June 26, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA WATENDAJI KUSIMAMIA MIRADI KIKAMILIFU

    June 18, 2025
  • KAMATI YA USALAMA SENGEREMA YAKAGUA MIRADI BUCHOSA

    June 12, 2025
  • Waziri Mkuu Apongeza Mradi wa jengo la Utawala,Aweka jiwe la msingi

    May 19, 2025
  • Angalia zote

Video

UTOAJI WA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUCHOSA
Video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Mpango Mkakati Wa Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Mkoa wa Mwanza
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA)
  • Wizara ya Kilimo

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Buchosa District Council

    Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA

    Simu: 0759941297

    Simu ya kiganjani: 0765029662

    Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa