• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe |
Buchosa District Council
Buchosa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Misitu
    • Biashara
    • Ushirika
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Telesenta
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi idhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Mwenyekiti UWT aridhishwa na kupongeza miradi ya Maendeleo Wilayani Buchosa

Posted on: August 6th, 2024

Mwenyekiti wa UWT Taifa aridhishwa na kupongeza Miradi ya Maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa Mkoani Mwanza.

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama cha Wanawake wa Chama cha Mapinduzi Tanzania Bi.Mary Chatanda leo 06,Agosti,2024 ametembelea na kukagua Mradi wa Kituo cha Afya Nyakasungwa kilichopo Kata ya Nyakasungwa ambapo  ameridhishwa na hatua ya ujenzi wa kituo hicho ambacho kimetumia fedha za mapato ya ndani.

Mwenyekiti wa UWT amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa Bw.Benson P.Mihayo kwa kusimamia kikamilifu ukusanyaji wa mapato kupelekea kujenga Kituo cha Afya Cha Nyakasungwa ambacho kipo katika hatua ya ukamilishaji ikiwa pamoja upakaji wa rangi,milango na madirisha.

“Tunawapongeza sana sana kwa kazi nzuri mnayofanya,hongereni sana,Nampongeza Mhe Diwani,Mkurugenzi Mtendaji kwa kusimamia kikamilifu ukusanyaji wa mapato”Amesisitiza Bi.Chatanda.

Aidha Bi.Chatanda amesema na kufafanua kwamba Serikali inatoa fedha nyingi kwa ajili ya kuleta Miradi ya Maendeleo ikiwemo miradi ya afya ili wananchi waweze kupata huduma bora na kwa wakati.

Kwa upande Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe.Senyi Ngaga akiongea na wananchi wa Kijiji cha Luchili Kata ya Nyazenda amefafanua kwamba Serikali ya awamu ya sita imekuwa ikitekeleza miradi mingi ya Maendeleo hususani kwenye Sekta ya afya, Elimu,Maji na Miundombinu ya barabara ambapo amesema barabara ya kutoka Sengerema kwenda Nyehunge itakuwa kwenye kiwango cha lami.

“Najua hilo ni hitaji kubwa la wanabuchosa wote kwa sababu inatuanganisha” Amesema Mkuu wa Wilaya ya Sengerema.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa amesema kwamba kupitia Waheshimiwa Madiwani pamoja menejimenti na watumishi kwa ujumla wake wanashirikiana kuhakikisha mapato yanapatikana na kutumika kwa usahihi sambamba na kutoa motisha kwa watumishi ambao wanafakazi kwa bidii na  uadilifu katika Halmasahauri ya Wilaya ya Buchosa.

Hata hivyo,Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa ilitenga fedha kiasi cha shilingi 150,000,000/= kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kutoka fedha mapato ya ndani kwa ajili ya kuanza ujenzi wa miundombinu ya kituo cha Afya katika Kata ya Nyakasungwa kwa kutekeleza ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) ambapo ujenzi unatarajiwa kukamilika mwezi 8 mwaka huu,mpaka sasa fedha iliyotumika ni shilingi 83,648,040/=.

Wananchi wa Kijiji cha Luchili na maeneo jirani wamejitokeza kwa wingi kwenye ziara ya Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Taifa Bi.Mary Chatanda leo,ambapo amewataka kujitokeza kushiri kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kuwachagua Viongozi wanaowataka.


Mwonekano wa jengo la Kituo cha Afya Nyakasungwa ambapo mpaka sasa umegharimu kiasi cha fedha shilingi 83,648,040/= kitakapokamilika kitasaidia kutoa huduma kwa wananchi wa Nyakasungwa na maeneo jirani.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA UMMA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 26, 2024
  • MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KWA AJILI YA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA(BVR)-2024 August 02, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA July 17, 2024
  • TANGAZO LESENI ZA BIASHARA 2024 July 10, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • DC Ngaga asisitiza Mahusiano mazuri kazini Buchosa

    April 03, 2025
  • DED Benson Mihayo awataka watumishi kushirikana katika ukusanyaji Buchosa

    March 27, 2025
  • Angalia zote

Video

UTOAJI WA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUCHOSA
Video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Mpango Mkakati Wa Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Mkoa wa Mwanza
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA)
  • Wizara ya Kilimo

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Buchosa District Council

    Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA

    Simu: 0759941297

    Simu ya kiganjani: 0765029662

    Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa