• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe |
Buchosa District Council
Buchosa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Misitu
    • Biashara
    • Ushirika
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Telesenta
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi idhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Maambukizi ya VVU yapungua Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

Posted on: December 1st, 2024

Siku ya UKIMWI duniani huadhimishwa tarehe 1 Disemba kila mwaka ili kueneza ufahamu wa ugonjwa wa UKIMWI unaosababishwa na uambukizi wa virusi vya UKIMWI.

Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yamefanyika leo tarehe 01,Disemba 2024 Kijiji cha Bugani  Kata ya Bulyaheke katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa, ambapo mgeni rasmi alikuwa Diwani wa Kata ya hiyo  Mhe.Ngele Nyuki Bageti ameeleza na kufafanua kwamba lengo la maadhimisho hayo ni kuhamasisha jamii kuendelea kushiriki kwenye ajenda ya udhibiti UKIMWI ambayo ni ajenda ya kidunia, kutathmini muelekeo wa kudhibiti Virusi vya UKIMWI nchini na kutafakari changamoto mafanikio na uimarishaji wa mikakati mbalimbali ya udhibiti wa Virusi vya UKIMWI(VVU).

Aidha Mhe.Bageti amesema kwamba hali ya maambukizi ya UKIMWI kwa Halmashauri ya Buchosa imepungua na kufikia asilimia 1.7 kwa mwaka 2024 ukilinganisha na mwaka 2023 ambapo kiwango cha maambukizi kilikuwa ni asilimia 2.6 hivyo Halmashauri imefanya kazi kubwa kupunguza maambukizi mapya ya ukimwi.

“Nitoe rai kwa wananchi wote wa Halmashauri ya Buchosa bila kujali rika zao waendelee kujilinda kwani kwa kufanya hivyo wataendelea kuwa na afya njema na kuendelea kufanya shughuli za maendeleo kwa ajili ya familia zao na Taifa kwa ujumla”amesisitiza Mhe.Bageti.

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii Bw.Florian Mkangala ameeleza kwamba katika kupambana na kuzuia maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI,afua mbalimbali zimetekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa ikiwa ni pamoja na Kutoa Elimu kwa wananchi,ushauri nasaha na upimaji,dawa kinga (PEP,PreP),ugawaji wa kondomu pamoja na Tohara.

Hata hivyo Halmashauri katika kutekeleza afua za VVU/UKIMWI imekua ikishirikiana na Wizara ya Afya na wadau mbalimbali kama vile ICAP,ELECT-ELVD,(TB HIV),AMERICARE (PMTCT) lengo kuu ni kufikia malengo ya millennia ya 95 tatu ikifikapo 2030.

Maadhimisho hayo yameaambatana na shughuli mbalimbali zikiwemo upimaji wa VVU na utoaji ushauri nasaha,utoaji wa elimu ya magonjwa yasiyoambukiza, Elimu ya Lishe pamoja na Upimaji wa hiari wa VVU (Virusi vya Ukimwi).

Kaulimbiu ya maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani kwa mwaka 2024 inasema 'Chagua njia sahihi tokomeza UKIMWI'.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA UMMA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 26, 2024
  • MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KWA AJILI YA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA(BVR)-2024 August 02, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA July 17, 2024
  • TANGAZO LESENI ZA BIASHARA 2024 July 10, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • DC Ngaga asisitiza Mahusiano mazuri kazini Buchosa

    April 03, 2025
  • DED Benson Mihayo awataka watumishi kushirikana katika ukusanyaji Buchosa

    March 27, 2025
  • Angalia zote

Video

UTOAJI WA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUCHOSA
Video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Mpango Mkakati Wa Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Mkoa wa Mwanza
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA)
  • Wizara ya Kilimo

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Buchosa District Council

    Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA

    Simu: 0759941297

    Simu ya kiganjani: 0765029662

    Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa