• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe |
Buchosa District Council
Buchosa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Misitu
    • Biashara
    • Ushirika
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Telesenta
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi idhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Kamati ya Siasa CCM Sengerema yaridhishwa na utekelezaji wa Miradi Buchosa

Posted on: February 3rd, 2025

Kamati ya Siasa CCM Wilaya ya Sengerema yaridhishwa na kupongeza utekelezaji wa Miradi ya sekta ya Afya na Miundombinu ya ujenzi wa VETA inayoendelea kutekelezwa katika Halmashauri ya Buchosa Mkoani Mwanza.

Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe, Rais,Dkt. Samia Suluhu Hassan katika juhudi za kuboresha na kukuza Uchumi wa Wananchi imeendelea kuleta neema katika sekta ya Elimu, Maji na miundombinu ya barabara kwa kutoa fedha za kujenga miradi na hatua za ukamilishaji zinaendelea vizuri.

Kamati ya Siasa Wilaya ya Sengerema CCM ikiongozwa na Mwenyeki wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya Mhe.Marco Makoye (DM) tarehe 03.Februari,2025 imetembelea na Kukagua  Kituo cha Afya Lushamba ambacho kina jumla ya majengo Matano (5) Jengo la wagonjwa wanje (OPD),Jengo la Maabara,Jengo la Mama na mtoto,jengo la Upasuaji,na nyumba moja ya familia mbili, na kuonyeshwa kuridhishwa na ujenzi wa Kituo hicho ambacho kimegharimu shilingi 648,364,940.70 fedha kutoka Serikali kuu kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF,ambapo Kituo hicho hapo awali kilijulikana kama Zahanati ya Lushamba,kilianza kutoa huduma rasmi kama Kituo cha Afya mnamo Januari 2024.

Wakati huo huo, Wajumbe wa Kamati ya Siasa Wilaya ya Sengerema pia wamekagua  ujenzi wa Chuo cha Ufundi VETA kinachojengwa kwa fedha kutoka Serikali Kuu katika Kijiji cha Kayenze Kata ya Nyehunge Halmashauri ya Buchosa, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Sengerema Mhe,Makoye (DM) amesema kwamba Miradi ya Maendeleo inatakiwa kukamilika kwa wakati ili wananchi waweze kunufaika Miradi hiyo katika Halmashauri ya Buchosa.

Aidha Kamati hiyo ilipata wasaa wa kutembelea wagonjwa ambao walikuwa wanapatiwa huduma ya matibabu katika Kituo hicho na kupatiwa pole kama motisha kwa wagonjwa hao, sambamba na kusherekea miaka 48 ya Chama cha Mapinduzi kwa vitendo ambapo miti kadhaa ilipandwa kama kumbukumbu katika eneo la kituo hicho.

Kwa Upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendai wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa Dkt.David Mndeba ambaye pia ni Mganga Mkuu wa Halmasahuri ya Buchosa ameeleza na kufafanua kwamba Serikali ya awamu ya Sita imetoa fedha kiasi cha shilingi 300,000,000/=kwa ajili ya kununua vifaa tiba mbalimbali kutoka bohari ya dawa (MSD) kununuliwa kwa vifaa tiba vimesaidia kuboresha huduma mbalimbali kama ultrasound (uchunguzi kwa njia ya kioo) na huduma za upasuaji.

Hata hivyo Dkt Mndeba ameongeza kuwa walifanikiwa kupokea vifaa mbalimbali kutoka Global Fund vikiwemo Vitanda 15, Magodoro 15, mashuka 60 na meza za kwenye vitanda hivyo.

Sambamba na hayo ameishukuru Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Sengerema kwa kufanya ziara na kukagua maendeleo ya miradi katika Sekta ya Afya na kuwaomba waendelee kufanya ufuatiliaji huo ili kuwezesha miradi hiyo kukamilika kwa wakati.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA UMMA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 26, 2024
  • MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KWA AJILI YA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA(BVR)-2024 August 02, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA July 17, 2024
  • TANGAZO LESENI ZA BIASHARA 2024 July 10, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • DC Ngaga asisitiza Mahusiano mazuri kazini Buchosa

    April 03, 2025
  • DED Benson Mihayo awataka watumishi kushirikana katika ukusanyaji Buchosa

    March 27, 2025
  • Angalia zote

Video

UTOAJI WA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUCHOSA
Video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Mpango Mkakati Wa Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Mkoa wa Mwanza
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA)
  • Wizara ya Kilimo

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Buchosa District Council

    Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA

    Simu: 0759941297

    Simu ya kiganjani: 0765029662

    Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa