• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe |
Buchosa District Council
Buchosa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Misitu
    • Biashara
    • Ushirika
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Telesenta
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi idhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC Sengerema awataka Madiwani kuongeza juhudi kusimamia Ukusanyaji Mapato katika Halmashauri ya Buchosa

Posted on: August 22nd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Sengerema aipongeza Halmashauri ya Buchosa kwa kuvuka lengo la Ukusanya wa Mapato kwa mwaka wa fedha 2023/2024 na kuwataka Madiwani kuendelea kusimamia kikamilifu ukusanya wa mapato  kwa mwaka mpya wa fedha 2024/2025.

Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe.Senyi Ngaga ameyasema hayo jana Agosti 21, 2024 kwenye kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa la kujadili taarifa za robo ya nne Aprili hadi Juni 2024, ambapo amewapongeza Waheshimiwa Madiwani na Menejimenti kwa kushirikiana pamoja katika kusimamia kikamilifu ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa.

Aidha Bi.Ngaga ameipongeza Halmashauri kuwa kuendelea kusimamia vizuri miradi ya Maendeleo pamoja na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ambapo imetekelezwa kwa sehemu kubwa,hivyo ametoa rai kwamba kwa Miradi ambayo bado haijakamilika wahakikishe inakamilika kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma.

Kwa upande mwingine Mkuu huyo wa Wilaya ya Sengerema amewakumbusha Madiwani kuwahimiza wananchi kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 2024.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Buchosa Mhe.Idama Kibanzi ameeleza na kufafanua kwamba kama Halmashauri wamejipanga kikamilifu kwa mwaka mpya wa fedha 2024/2025 kusimamia ukusanyaji wa mapato na matumizi ya fedha za Serikali katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa.

Sambamba na hiyo, Mhe. Kibanzi amesema kwa niaba ya Waheshimiwa Madiwani watahakikisha wanasimamia kikamilifu fedha zote za miradi ya Maendeleo kwa kila Kata ikiwemo miradi ya Afya,Elimu na Maji ili wananchi waweze kunufaika na miradi hiyo kwa wakati.

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi  Wilaya ya Sengerema Bi.Waridi J.Mngumi  ametoa wito kwa Waheshimiwa Madiwani  kwenda kuwahamisha wananchi kujitokeza kushiriki kwenye uboreshaji wa Daftari la kudumu la mpiga kura ili baadaye waweze kushiri kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Naye Diwani wa Viti Maalumu Kata ya Kazunzu Mhe.Zena J.Mbiso amemshukuru Rais wa Jumhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuleta fedha nyingi za mradi mkubwa wa maji Kata ya Kazunzu na maeneo mengine ya Halmashauri ya Buchosa pamoja na miradi mingine ya Afya,Elimu na Miundombinu ya barabara.

Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe, Senyi Ngaga akitoa maelekezo katika kikao cha Baraza la Madiwani cha robo ya nne mwaka wa fedha 2023/2024 jana katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri,ambapo amewapongeza waheshimiwa Madiwani pamoja na Watumishi kwa ushirikiano katika kufanya kazi kwa pamoja.

Waheshimiwa Madiwani wakishiriki na kutoa maoni na ushauri katika kikao cha Baraza la Madiwani hapo jana katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri kwa robo ya nne Aprili hadi Juni 2024.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA UMMA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 26, 2024
  • MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KWA AJILI YA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA(BVR)-2024 August 02, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA July 17, 2024
  • TANGAZO LESENI ZA BIASHARA 2024 July 10, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • DC Ngaga asisitiza Mahusiano mazuri kazini Buchosa

    April 03, 2025
  • DED Benson Mihayo awataka watumishi kushirikana katika ukusanyaji Buchosa

    March 27, 2025
  • Angalia zote

Video

UTOAJI WA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUCHOSA
Video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Mpango Mkakati Wa Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Mkoa wa Mwanza
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA)
  • Wizara ya Kilimo

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Buchosa District Council

    Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA

    Simu: 0759941297

    Simu ya kiganjani: 0765029662

    Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa