• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe |
Buchosa District Council
Buchosa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Misitu
    • Biashara
    • Ushirika
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Telesenta
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi idhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Buchosa yaadhimisha Siku ya Uhuru Tanzania Bara kwa Kupanda miti na Kufanya Usafi

Posted on: December 9th, 2024

Disemba 9, kila Mwaka Tanzania Bara husherehekea Siku ya Uhuru wa Tanganyika uliopatikana Disemba 9, 1961 kutoka kwa Uingereza.

Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa leo tarehe 9 Disemba,2024 imeadhimisha siku ya Uhuru wa Tanzania Bara katika Kata ya Nyakaliro kwa kufanya usafi wa mazingira na kupanda miti ambapo takribani miche 520 imepandwa katika Shule ya msingi Lumeya iliyopo Kata ya Nyakaliro.

Akiongea katika maadhimisho hayo Katibu Tawala wa Wilaya ya Sengerema Bw.Cuthbert Midala ambaye alimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Sengerema amesema kuwa  maadhimisho hayo yamejikita zaidi katika kufanya shughuli za kijamii kama kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira ambapo kwa Wilaya ya Sengerema imefanya usafi katika hospitali ya Wilaya ya Sengerema na kwenye vituo vya na kupanda miti,kwaHalmashauri ya Buchosa imefanya usafi wa mazingira katika hospitali ya Wilaya Isaka iliyopo Kata ya Nyehunge pamoja na upandaji miti.

Aidha Bw.Midala ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutunza mazingira kwa kufanya usafi wa mazingira pamoja na kupanda miti na kuilinda ili ilete manufaa kwa wananchi na vizazi vijavyo.

Kwa upande Mhifadhi Mkuu wa TFS Sengerema Bw.Steven Odongo Oyugi ameeleza na kufafanua kwamba wao kama TFS wanatoa elimu kwa wananchi namna nzuri ya kupanda na kuitunza miti na kutunza mazingira kwa ujumla wake pamoja na kugawa miche mbalimbali, ambapo ametoa wito kwa wananchi Kwenda kuchukua miche kwa ajili kupanda kwa manufaa ya wananchi kwa kujipatia kipato.

Vilevile Diwani wa Kata ya Nyakaliro Mhe.Paulo Kabugwe ametoa shukrani za pekee kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Buchosa na Kata ya Nyakaliro.

Naye mkazi wa Kijiji cha Lumeya Bw.Edward Mazengo ameomba uongozi wa TFS kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu umuhimu wa kutunza mazingira hasa upandaji wa miti ili kunusuru majangwa ambayo yanaendelea kutokea katika maeneo yanayowazunguka.

Katika maadhimisho hayo wananchi wamejitokeza kwa wingi katika kuadhimisha miaka 63 ya Uhuru Tanzania Bara ambapo kauli mbiu inasema “Uongozi Madhubuti na Ushirikishwaji wa Wananchi ni Msingi wa Maendeleo yetu”.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA UMMA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 26, 2024
  • MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KWA AJILI YA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA(BVR)-2024 August 02, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA July 17, 2024
  • TANGAZO LESENI ZA BIASHARA 2024 July 10, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • DC Ngaga asisitiza Mahusiano mazuri kazini Buchosa

    April 03, 2025
  • DED Benson Mihayo awataka watumishi kushirikana katika ukusanyaji Buchosa

    March 27, 2025
  • Angalia zote

Video

UTOAJI WA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUCHOSA
Video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Mpango Mkakati Wa Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Mkoa wa Mwanza
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA)
  • Wizara ya Kilimo

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Buchosa District Council

    Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA

    Simu: 0759941297

    Simu ya kiganjani: 0765029662

    Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa