• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe |
Buchosa District Council
Buchosa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Misitu
    • Biashara
    • Ushirika
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Telesenta
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi idhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Baraza la Wafanyakazi lapitisha Bajeti Bilioni 42.4 kwa mwaka wa fedha 2025/2026 Wilayani Buchosa

Posted on: January 28th, 2025

Baraza la Wafanyakazi la Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa lajadili na kupitisha mapendekezo ya Bajeti ya Mapato na Matumizi ya shilingi Bilioni 42.4 kwa mwaka wa fedha 2025/2026 Wilayani Buchosa Mkoani Mwanza.

Kikao maalum cha Baraza la Wafanyakazi kwa ajili kutoa mapendekezo ya bajeti katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ambapo Mwenyekiti wa kikao hicho ambaye pia ni Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Buchosa Bw. Adolf Ritte ameeleza kwamba ni halali kwa kila mfanyakazi kutimiza wajibu wake na kusisitiza ushirikiano ili kuhakikisha wanafikia adhima na malengo yaliyowekwa na kuwaomba Watumishi waendelee kutekeleza majukumu kwa kuzingatia Bajeti iliyopitishwa.

Bw. Adolph amefafanua na kueleza kuwa kikao hicho ni maalum kwa ajili ya kupitia,kujadili na kufanya tathmini ya utendaji kazi ambapo kila mfanyakazi ana haki katika utekelezaji wa majukumu na stahiki anapowajibika kutimiza malengo yaliyopangwa kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Awali akiwasilisha rasimu ya Bajeti ya mwaka 2025/2026 Afisa Mipango wa Halmashauri Bw.Deogratius Ihengelimo  kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa amefafanua kwamba katika rasimu hiyo ya Bajeti kiasi cha shilingi 4,311,199,797.00/= ni fedha zitokanazo na vyanzo vya Mapato ya ndani ya Halmashauri ,kiasi cha shilingi. Bilioni 25,538,180,000/= ni fedha ya mishahara ya Watumishi, na kiasi cha shilingi Bilioni 2,107,638,000/= ikiwa ni ruzuku ya uendeshaji (OC) na kiasi cha shilingi Bilioni 10,458,340,000/= ni kwa ajili ya kutekeleza Miradi ya Maendeleo na fedha zote ni kutoka Serikali kuu.

Aidha Bw.Ihengelimo ameeleza kuwa pamoja na kuwepo kwa rasimu ya bajeti hiyo ofisi ya Mipango na Uratibu imeahidi kutekeleza na kufanyia kazi mapendekezo na maadhimio ya kikao hicho ikiwa ni pamoja na kuendeleza ushirikiano ili kuhakikisha kuwa na maendeleo chanya katika jamii ndani ya Halmashauri ya Buchosa.

Hata hivyo kupitia kikao hicho cha Baraza la Wafanyakazi, wajumbe walipata wasaa wa kupitia na kujadili pamoja na kutoa maoni  yao juu ya  Bajeti hiyo na kupongeza namna ulivyoandaliwa kitaalamu.


Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA UMMA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 26, 2024
  • MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KWA AJILI YA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA(BVR)-2024 August 02, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA July 17, 2024
  • TANGAZO LESENI ZA BIASHARA 2024 July 10, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • DC Ngaga asisitiza Mahusiano mazuri kazini Buchosa

    April 03, 2025
  • DED Benson Mihayo awataka watumishi kushirikana katika ukusanyaji Buchosa

    March 27, 2025
  • Angalia zote

Video

UTOAJI WA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUCHOSA
Video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Mpango Mkakati Wa Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Mkoa wa Mwanza
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA)
  • Wizara ya Kilimo

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Buchosa District Council

    Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA

    Simu: 0759941297

    Simu ya kiganjani: 0765029662

    Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa