• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe |
Buchosa District Council
Buchosa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Misitu
    • Biashara
    • Ushirika
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Telesenta
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi idhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Baraza la Madiwani la ridhishwa na taarifa za hesabu za mwisho kuishia Juni 30,2024 Wilayani Buchosa

Posted on: August 28th, 2024

Bazara za Madiwani la ridhishwa na kupongeza taarifa za hesabu za mwisho kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2024 katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa.

Pongezi hizo zimetolewa leo 28,Agosti,2024 ambapo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa na diwani wa Kata ya Nyazenda Mhe.Idama Kibanzi ameeleza na kufafanua  kwamba Baraza la Madiwani katika kikao chake cha kujadili taarifa za hesabu za mwisho kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2024 limeridhika na taarifa hiyo ambayo imeeleza kila kitu kwa undani na kwa ufasaha kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya uandaji wa hesabu za Sekta za Umma.

“Kwa mwaka huu naona hesabu zetu ziko salama,nawashukuru Madiwani,Mkurugenzi Mtendaji na menenjimenti kwa namna ya pekee unavyoonesha ushirikiano kwa waheshimiwa Madiwani”.Ameongeza Mwenyekiti wa Halmashauri ya Buchosa Mhe.Kibanzi.

Aidha Bw.Kibanzi amesema kwamba taarifa za hesabu kwa mwaka wa fedha 2023/2024 zimejumuisha mapato,matumizi,mali za kudumu,madeni,mali zilizo salia stoo na salio la fedha kwenye akaunti za Halmashauri,shule,Zahati,Vituo vya Afya,Kata na Vijiji.

Katika Hatua nyingine Baraza la Madiwani kwa ujumla wake limeridhia na kumpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa Bw.Benson Mihayo kwa namna anavyosimamia na kushirikiana na Madiwani pamoja na namna taarifa ilivyoandaliwa kitaalamu kwa kuzingatia vigezo vya Kimataifa na kujumuisha vitu vya msingi ikiwa pamoja na madeni ya watumishi na wazabuni wanaoidai katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu mweka Hazina CPA Justice N.Shemakange amesema uandaji wa hesabu za kuishia 30/06/2024 umezingatia viwango vya kimataifa vya uandaji wa hesabu za Sekta Umma,sheria za fedha ,sharia za manunuzi ya umma ya mwaka 2011 na kanuni zake za 2013 na 2016 na sheria ya Serikali za mitaa ya mwaka 1982 kama ilivyorekebishwa mwaka 2000.

Hata hivyo,Bw.Shemakange ametoa shukrani za pekee kwa menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa na Kitengo cha fedha  kwa ushirikiano wa dhati walioonesha kwa kipindi cha maandalizi ya hesabu hizo zilizoishia Juni,30,2024.

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa leo limejadili na kuridhwisha na taarifa ya hesabu za mwisho kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30,2024 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.


Kaimu Mkuu mweka Hazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa CPA Justice N.Shemakange akiwasilisha taarifa za hesabu za mwisho wa mwaka ambapo amesema uandaji wa hesabu za kuishia 30/06/2024 umezingatia viwango vya kimataifa.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA UMMA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 26, 2024
  • MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KWA AJILI YA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA(BVR)-2024 August 02, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA July 17, 2024
  • TANGAZO LESENI ZA BIASHARA 2024 July 10, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • DC Ngaga asisitiza Mahusiano mazuri kazini Buchosa

    April 03, 2025
  • DED Benson Mihayo awataka watumishi kushirikana katika ukusanyaji Buchosa

    March 27, 2025
  • Angalia zote

Video

UTOAJI WA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUCHOSA
Video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Mpango Mkakati Wa Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Mkoa wa Mwanza
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA)
  • Wizara ya Kilimo

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Buchosa District Council

    Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA

    Simu: 0759941297

    Simu ya kiganjani: 0765029662

    Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa