• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe |
Buchosa District Council
Buchosa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Misitu
    • Biashara
    • Ushirika
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Telesenta
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi idhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Baraza la Madiwani Buchosa wapata Mafunzo namna bora ya Ukusanyaji Mapato

Posted on: December 6th, 2024

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa limefanya ziara ya Kikazi,katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza yenye lengo la kujifunza masuala mbalimbali ya Uendeshaji wa Halmashauri ikiwa ni pamoja na ukusanyaji Mapato.

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa wakiwa wameambatana na wataalamu mbalimbali katika wa Halmashauri hiyo wamefanya ziara leo tarehe 6,Desemba,2024 katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa lengo la kujifunza namna ya kuongeza mapato kupitia Miradi mbalimbali.

Akiongea wakati wa Mafunzo hayo katika ukumbi wa mikutano Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Bw. Erick Mvati ameeleza kuwa Halmashauri ya Jiji la Mwanza imebua vyanzo mbalimbali vya mapato kuhakikisha wanakusanya mapato ya kutosha ili kutekeleza Miradi ya maendeleo pamoja na kuwashirikisha wananchi katika kutekeleza miradi ya maendeleo ambapo kwa sasa jamii imejengewa uwezo  juu ya uibuaji wa miradi ambayo wataweza kuitekeleza na kuikamilisha bila kutegemea usaidizi kutoka Serikalini.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa Mhe.Idama Kibanzi amempongeza Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza pamoja na watendaji wote kwa kuweza kushirikiana vyema katika kukuza mapato ya Jiji pamoja na usimamizi na utekelezaji mzuri wa miradi huku akiahidi kwenda kufanyia kazi yote waliyojifunza.

“Kipekee naomba kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa mapokezi mazuri kutoka kwenu na pia kujitoa kwenu kutupatia Elimu hii ya ukusanyaji wa kodi na utekelezaji wa Miradi, Hakika ziara yetu imekua yenye mafanikio makubwa kwani tumejifunza mambo mengi na mazuri na tutayafanyia kazi pindi tutakaporejea Buchosa“Amesema Mhe. Kibanzi.

Sambamba na hilo, Waheshimiwa hao Waliweza kujifunza mbinu mbalimbali za uwekezaji ambapo kwa Jiji la Mwanza wamewekeza kwenye ujenzi wa soko kuu la kisasa,Stendi kuu ya kisasa ya mabasi Nyegezi,Ujenzi wa Shule za Medium pamoja na Sekta Uvuvi    ambayo ni Chachu ya kuongeza mapato kwa Jiji hilo kwani muundo wa ujenzi wa masoko hayo ni rafiki kupelekea Halmashauri kupata mapato zaidi.

Vilevile Madiwani na watalamu hao Waliweza kutembelea shamba la samaki eneo la Luchelele Kisoko kujifunza namna ufugaji wa Samaki kwa kutumia vizimba ambapo kupitia ufugaji huo mapato ya Halmashauri ya Jiji yanaongezeka.

Katika hatua nyingine Madiwani wametoa shukrani za dhati kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa kwa kuandaa ziara ya mafunzo ya ukusanyaji wa mapato ya ndani kupitia vyanzo mbalimbali na namna ya usimaiaji wa miradi ya kimkakati inayotekelezwa kwenye Halmashauri hizo.

Naye mkazi wa Luchelele Bw.Fikiri Elias ambaye mnufaika wa mradi wa ufugaji Samaki kwa kutumia vizimba amesema mradi huo umemsadia kujiajiri ambapo kupitia mazao ya Samaki anapata faida na hivyo hafikiri kuajiriwa sehemu nyingine.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA UMMA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 26, 2024
  • MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KWA AJILI YA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA(BVR)-2024 August 02, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA July 17, 2024
  • TANGAZO LESENI ZA BIASHARA 2024 July 10, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • DC Ngaga asisitiza Mahusiano mazuri kazini Buchosa

    April 03, 2025
  • DED Benson Mihayo awataka watumishi kushirikana katika ukusanyaji Buchosa

    March 27, 2025
  • Angalia zote

Video

UTOAJI WA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUCHOSA
Video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Mpango Mkakati Wa Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Mkoa wa Mwanza
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA)
  • Wizara ya Kilimo

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Buchosa District Council

    Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA

    Simu: 0759941297

    Simu ya kiganjani: 0765029662

    Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa