• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe |
Buchosa District Council
Buchosa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Misitu
    • Biashara
    • Ushirika
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Telesenta
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi idhinishwa
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Mwenge wa Uhuru 2024 wazindua,kukagua na Kuweka jiwe la Msingi Miradi ya Maendeleo Buchosa

Posted on: October 7th, 2024

Mwenge wa Uhuru kitaifa wazindua,kukagua na kuweka jiwe la msingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo yenye thamani ya Bilioni 2.9 katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa.

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ndg. Godfrey Eliakim Mnzava jana tarehe 06 Oktoba, 2024 amezindua,kukagua na kuweka jiwe la msingi katika miradi 6 ambayo ni Mradi wa Vyumba viwili vya madarasa Nyehunge,Mradi wa umwagiliaji Sukuma,Mradi wa Kituo cha Afya Nyakasungwa,Mradi wa upandaji miti,Mradi wa Vijana na mradi wa Maji katika Kijiji cha Kasela Kata ya Nyakaliro.

Ndg. Godfrey Eliakim Mnzava amezindua mradi wa skimu ya umwagiliaji iliyojengwa kwa shilingi Bilioni 2. 4 kupitia tume ya taifa ya umwagiliaji kwenye kijiji cha Sukuma kilichopo Kata ya Bukokwa.

Akizungumza na wananchi wa Sukuma, Magurukenda na maeneo ya jirani, ndugu Mnzava ameipongeza serikali kwa kutekeleza ujenzi wa miundombinu hiyo na amebainisha kuwa itawasaidia wakulima kuongeza uzalishaji kwa kufanya shughuli hizo katika kipindi chote cha mwaka pasipo kusubiri mvua.

Bw.Mzanva  amewaondoa hofu wananchi kwamba mradi huo sio kwa ajili ya wawekezaji na katika hilo amewahakikishia kuwa mradi huo ni kwa ajili ya wananchi na kwamba serikali ya awamu ya sita imedhamiria kuwainua wananchi wake kiuchumi.

"Mradi huu ni kwa ajili ya wananchi sio wawekezaji, naomba mpuuze maneno na minong'ono inayosema kwamba mradi huo umetekelezwa kwa ajili ya wawekezaji tumieni fursa hii kuongeza uzalishaji kwenye mazao ya chakula, matunda na mbogamboga." Amesema Kiongozi wa mbio za Mwenge.

Hata hivyo Mbio za Mwenge wa uhuru umezindua madarasa 2 na matundu 6 ya vyoo katika shule ya awali na msingi Nyehunge iliyotekelezwa na serikali kwa thamani ya shilingi milioni 55.8 kupitia mradi wa GPE LANES kabla ya kuweka jiwe la msingi kwenye Zahanati ya Nyakasungwa ambapo Milioni 250 za mapato ya ndani yakijenga majengo ya OPD na maabara.

Katika hatua nyingine Mwenge wa Uhuru umezindua mradi wa maji kwenye kijiji cha Kasela wenye uwezo wa kuzalisha lita milioni moja kwa siku wenye thamani ya Milioni 218 ambapo kiongozi wa mbio hizo amewapongeza wasimamizi (RUWASA) kwa kuongeza hali ya upatikanaji wa maji safi kutoka 10% hadi 85%.

Mbio za Mwenge zimekimbizwa kwa umbali wa kilomita 68.6 ambapo umezindua,kukagua na kuweka jiwe la msingi miradi ya maendeleo yenye thamani ya shilingi Bilioni 2.9 katika Halmashauri ya Wilaya ya buchosa.

Matangazo ya Kawaida

  • TANGAZO KWA UMMA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 26, 2024
  • MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KWA AJILI YA USAILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGAKURA(BVR)-2024 August 02, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA July 17, 2024
  • TANGAZO LESENI ZA BIASHARA 2024 July 10, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • Halmashauri ya Buchosa yapongezwa kupata Hati safi

    April 28, 2025
  • DC Ngaga asisitiza Mahusiano mazuri kazini Buchosa

    April 03, 2025
  • DED Benson Mihayo awataka watumishi kushirikana katika ukusanyaji Buchosa

    March 27, 2025
  • Angalia zote

Video

UTOAJI WA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA BUCHOSA
Video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Mpango Mkakati Wa Halmashauri

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Mkoa wa Mwanza
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA)
  • Wizara ya Kilimo

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Buchosa District Council

    Anuani: 44 Buchosa - SENGEREMA

    Simu: 0759941297

    Simu ya kiganjani: 0765029662

    Barua pepe: ded@buchosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki ©2017 Hamlashauri ya Wilaya ya Buchosa. Haki zote zimehifadhiwa